• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

VIJANA 58 WAHITIMU MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA KYERWA

Imewekwa tarehe: November 28th, 2023

Jumla ya vijana 58 wakike wakiwa 2 na wakiume 56 wamehitimu mafunzo ya jeshi la akiba maarufu kama mgambo ambao waliweka kambi katika Kata ya Kikukuru Wilaya ya Kyerwa tangu Julai  20, 2023.

Akizungumza katika sherehe ya kufunga mafunzo hayo leo Novemba 28, 2023, Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe amewataka vijana hao kuwa waadilifu na wazalendo kwa nchi yao pamoja na kuyatumia mafunzo waliyoyapata kwa maslahi yao na nchi nzima kwa ujumla.

“Tunatumaini kwamba mtatusaidia vyema katika kupunguza uhalifu. Tunategemea kwamba mtaungana na wenzenu ambao walishapata mafunzo na kwa kusaidiana na majeshi mengine ili kusaidia Wilaya ya Kyerwa ibaki salama, amani na utulivu. Kwa mafunzo mliopewa tunaamini kwamba sasa Kyerwa inaenda kuwa na utulivu.” Amesema Msofe.

Aidha kutokana sababu ya baadhi ya vijana kushindwa kujiunga na mafunzo hayo kwa kukosa kigezo cha kuwa na elimu ya msingi. Mkuu wa Wilaya ametoa rai kwa jamii kuwaandikisha watoto wao shule za msingi na wale wanaofaulu kuendelea na sekondari waandikishwe ili watoto wao wasijekukosa fursa mbalimbali hapo baadae.

Kwa upande wake Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Kyerwa SSGT Deomedes Rupia   amesema kuwa wahitimu hao wamehitimu mafunzo kwa kiwango kinachotakiwa na watakuwa tayari muda wote kulitumikia taifa lao.

Katika risala yao wahitimu wa mafunzo ya jeshi la akiba wamesema wamejengwa kikakamavu katika kujilinda wao wenyewe, raia na mali zao ikiwa ni pamoja na mafunzo ya matumizi ya silaha, ujanja wa porini, usomaji wa ramani, sheria za mgambo, kwata mbalimbali, elimu ya uraia, kuzuia na kupambana na rushwa, zima moto na mafunzo ya ujasiriamali.

Aidha wamesema mafunzo hayo yatasaidia kupunguza uhalifu katika jamii kwa kudhibiti wizi wa mazao, uvunjaji wa maduka na kupambana na magendo ya kahawa.

Naye DevothaTumainel, miongoni mwa wahitimu wa mafunzo hayo, ameipongeza na kuishukuru serikali kwa kupata mafunzo hayo na kuiomba serikali kuwapa kipaumbele cha kuwapa nafasi za kazi vijana wa kike wanaohitimu mafunzo hayo ili kuwavutia wengine kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Akiba kwa awamu ijayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO LA UTOAJI WA VITAMINI A NA UPIMAJI WA HALI YA LISHE KWA WATOTO WA UMRI KUANZIA MIEZI 6 HADI 59 November 27, 2023
  • TANGAZO LA MABADILIKO YA BEI YA USHURU WA MKUNGU WA NDIZI December 31, 2023
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • MNASTAHILI PONGEZI KWA USIMAMIZI, UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 07, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA KYERWA

    April 29, 2025
  • TUNAPASWA KUULINDA MUUNGANO WETU-DC. MSOFE

    April 26, 2025
  • ‘TAULO HIZI ZITAWASAIDIA WATOTO KUSOMA KWA UHURU NA UTULIVU’

    March 07, 2025
  • Tazama vyote

Video

Kamati ya siasa ukaguzi wa Miradi Kyerwa
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved