• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

RC KAGERA AFANYA ZIARA WILAYANI KYERWA

Imewekwa tarehe: August 5th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Kagera Hajjat Fatma Mwassa amefanya ziara Wilayani Kyerwa ikiwa ni mwendelezo wa kutembelea Wilaya zilizoko katika Mkoa wa Kagera ili kukagua na kupata taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Wilaya hizo.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa alitembelea miradi ya ujenzi wa jengo la utawala  la halmashauri na hospitali ya Wilaya Kyerwa ambayo ameridhishwa na kupongeza usimamizi mzuri wa miradi hiyo na kuwasisitiza wahusika wa miradi kuendelea kufanya kazi kwa kushirikiana na kusimamia miradi inayotekelezwa kwa fedha nyingi zinazotolewa na serikali ya awamu ya sita.

Aidha Mkuu wa Mkoa alifanya kikao cha ndani na wakuu wa idara na vitengo vya halmashauri na taasisi mbalimbali za serikali zilizopo wilayani Kyerwa na kupokea taarifa mbalimbali za usimamizi na utekelezaji wa shughuli za maendeleo zinazofanywa na wataalamu hao na baada ya hapo, alizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Nkwenda ambapo alipoka kero mbalimbali za wananchi na kuzitolea ufafanuzi.

Kero hizo zililenga katika uhaba wa maji safi na salama, changamoto ya barabara ya lami, umeme kutokufika katika baadhi ya vijiji na kukatika mara kwa mara, upungufu wa watumishi ikiwemo askari polisi, ukosefu wa namba na vitambulisho vya NIDA. Kero ambazo alizipokea na kutolewa ufafanuzi na kuahidi kuzifanyia kazi.

Vile vile amepokea maombi ya Nkwenda kuwa mji mdogo pamoja na kupatiwa chama cha ushirika cha Wilaya kwa ajili ya kukusanya kahawa na kuahidi kuyafanyia kazi maombi hayo kwa kushirikiana na wataalamu pamoja Mhe. Mbunge wa Jimbo la Kyerwa na pia kwa kuyafikisha sehemu husika ili kuongeza msukumo wa mambo hayo kushughulikiwa kwa haraka.

Pia katika hotuba yake Hajjat Fatma amewataka wananchi waache kutumia vibatali ambavyo hupelekea madhara makumbwa na mauaji ya kuungua moto kwani utumaduni wa watu wa Kagera hupenda kutandika nyasi ambazo ni rahisi kushika moto na kuwataka kutumia nishati mbadala. Pia na kuzingitia ulaji wa lishe bora, Pamoja na kudumisha umoja upendo na pia kuwataka wanakyerwa kujiandaa na mapokezi ya ujio wa mwenge wa uhuru 2023 na kushiriki kikamilifu.

Kuhusu Magendo ya kahawa amesema, “Serikali iko makini, wanaotorosha kahawa wanahujumu uchumi wa nchi, kwanza wanatukosesha fedha za kigeni, wanatukosesha ushuru wa mapato ya ndani zile asilimia ambozo tungepata hatupati, lakini pia wanarudisha nyuma maendeleo ya nchi yetu kwa hiyo tutakao wakamata watatumika kuwa mfono kwa wengine ambao wana nia ovu.”

Katika ziara hiyo mkuu wa mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa Mkoa Bw. Toba Nguvila na baadhi ya watalamu na kamati ya ulinzi na usalama mkoa ambao walipokelewa na wenyeji wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO LA UTOAJI WA VITAMINI A NA UPIMAJI WA HALI YA LISHE KWA WATOTO WA UMRI KUANZIA MIEZI 6 HADI 59 November 27, 2023
  • TANGAZO LA MABADILIKO YA BEI YA USHURU WA MKUNGU WA NDIZI December 31, 2023
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • MNASTAHILI PONGEZI KWA USIMAMIZI, UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 07, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA KYERWA

    April 29, 2025
  • TUNAPASWA KUULINDA MUUNGANO WETU-DC. MSOFE

    April 26, 2025
  • ‘TAULO HIZI ZITAWASAIDIA WATOTO KUSOMA KWA UHURU NA UTULIVU’

    March 07, 2025
  • Tazama vyote

Video

Kamati ya siasa ukaguzi wa Miradi Kyerwa
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved