• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

MZAZI KAMA HAJAMPELEKA MTOTO SHULE HATUA ZA KISHERIA ZITACHULIWA-MHE. HENERICO

Imewekwa tarehe: February 28th, 2025

Mkutano wa Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa umefanyika leo tarehe 28 Februari 2025 kwa ajili ya kujadili taarifa ya utekelezaji wa robo ya pili, kuanzia mwezi Oktoba hadi Desemba 2024/2025 katika ukumbi wa Halmashauri uliopo Rwenkorongo kata ya Kyerwa.

Akiongoza Mkutano huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa Mhe. Bahati Henerico amesisitiza Waheshimiwa Madiwani kushirikiana na wataalam wa Halmashauri kuhakikisha uandikishaji wa wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza waweze kuripoti na kujiunga katika shule walizopangiwa.

Hayo yamejiri baada ya kuwasilishwa taarifa ya hali ya kuripoti kwa wanafunzi na kuonekana baadhi ya shule kiwango cha kuripoti kipo chini huku Shule ya Sekondari Murongo ikiwa na 53% ya wanafunzi walioripoti hadi sasa.

“Huu mkakati wa watoto kwenda shule Waheshimiwa wajumbe kule tuko sisi viongozi wa Kata, twendeni sisi Madiwani tukahamasishe wananchi, watoto wote waende shule. Tukiacha maana yake tunazalisha shida.

“Baraza linaazimia, ikifika tarehe 15 Machi 2025 wanafunzi wote wawe wameripoti shule, Mkurugenzi waandikie walimu barua wape taarifa, watoto ambao hawajaripoti wanawajua kama kuna walioenda shule binafsi wajulikane, tuwaambie wananchi na wazazi wote wa Kyerwa kama mzazi au Mlezi hajampeleka mtoto shule hatua za kisheria zitachuliwa.” Amesema Mhe. Henerico.

Vile vile Mhe. Henerico ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya ya Kyerwa ikiwa ni pamoja na miradi ya afya, elimu, maji, barabara na umeme.

Aidha baraza limepatiwa taarifa ya uwepo wa timu ya wataalam ambayo inapita katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kyerwa kwa ajili ya kutoa elimu ya kudhibiti magonjwa ya kahawa ambayo yanavamia mibuni kwa kasi na kuhatarisha uzalishaji wa zao hilo kuu katika Wilaya ya Kyerwa na kuwataka Wahe. Madiwani na wananchi kutoa ushirikiano kwa wataalam hao.

Pia baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wakichangia katika baraza hilo wameelezea juu ya uwepo wa changamoto ya maji katika kata zao na kuomba zishughulikiwe ili kuwakwamua wananchi wa maeneo yao suala ambalo limechukuliwa na wahusika kwa ajili ya utekelezaji.


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI MBALIMBALI June 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • KYERWA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • NI SWALA LA KUAMUA TU, SISI WANAKYERWA HATUTAKI UCHAFU

    May 31, 2025
  • DC AFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

    May 29, 2025
  • TUSHIRIKIANE KUPAMBANA NA MAGENDO YA KAHAWA-DAS KYERWA

    May 14, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved