• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

MWENGE WA UHURU MWAKA 2024 WILAYANI KYERWA WAPITIA MIRADI YA SHILINGI BILION 8.5

Imewekwa tarehe: September 25th, 2024

Mwenge wa Uhuru 2024 umepokelewa leo  Septemba 25, 2024 Wilayani Kyerwa ambapo  umepitia jumla ya miradi ya maendeleo sita kwa kufungua miradi 2,  kuitembelea miradi 2, kuweka jiwe la msingi mradi1,  kuzindua mradi 1, na kufungua mradi 1. Miradi hiyo ya maendeleo ina thamani ya shilingi Bilioni 8.5

Miradi ambayo imetembelewa na mwenge wa uhuru   2024 ni ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye mahitahitaji maalum katika Shule ya Sekondari Mabira, ujenzi wa kiwanda cha kukoboa kahawa cha Kaderes-Kitwe, ujenzi wa barabara ya lami ya Rubwera Sekondari KM 1 iliyopo Rwenkorongo Kyerwa, ujenzi wa wodi ya magonjwa mchanganyiko katika kituo  cha Afya Nkwenda,ujenzi wa mradi wa maji wa Karongo Rwabwere na mradi wa Kikundi cha Bodaboda ni Ajira Kashanda katika Viwanja vya Standi ya Nkwenda.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa  Ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava, akizungumza kwa nyakati tofauti baada ya kutembelea na kukagua miradi hiyo, amesema miradi yote ambayo imepitiwa na mwenge  imetekelezwa kwa kiwango kinachoridhisha pia aliwapongeza wasimamizi wa miradi hiyo huku akiwaasa wananchi na wasiamamizi kuitunza  hiyo na kuiendeleza ili iweze kutoa huduma zilizokusudiwa kwa wananchi wa Wilaya ya Kyerwa.

Aidha, ndungu Mzava amefungua bweni la wanafunzi wenye mahitaji maalum ambalo limegharimu shilingi milioni 165,000,000 ambalo lenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi wa kiume 80 ambao wanasoma katika shule ya sekondari Mabira huku akifanya matendo ya huruma kwa kuwazawadia vifaa saidizi wanafunzi hao wenye mahitaji maalum.

Ndugu Mzava amempongeza Mwekezaji anayejenga kiwanda cha kukoboa kahawa cha Kaderes Kitwe ambacho kinajengwa na mwekezaji wa ndani Ndugu Leonard Kachebonaho na kusema kuwa kitatoa ajira kwa wananchi na kupunguza shughuli za magendo ambayo huchochewa na bai ndogo ya kahawa hivyo kiwanda hicho kitakuwa suluhisho la magendo kwa kuongeza thamani ya zao la kahawa.

Ndugu Mnzava akizungumza katika Kijiji cha Nyakatuntu baada ya kupokea taarifa ya maandalizi ya  uchaguzi ametoa wito kwa  viongozi na wadau mbalimbali kutumia nafasi zao na kufanya mikutano na wananchi kwa ajili ya kutoa elimu juu ya uchaguzi utakaofanyika tarehe 27 Novemba 2024 nchini na kuhakikisha kila mwananchi anakuwa na taarifa sahihi juu ya uchaguzi huo.

Aidha, ameipongeza Halmaahauri ya Wilaya ya Kyerwa kwa kutenga fedha za mapato ya ndani kuwezesha ujenzi wa wodi ya wanaume magonjwa mchanganiko iliyogharimu kiasi cha shilingi milioni 230,000,000 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo ambao utatoa huduma kwa wananchi na kusaidia ustawi wa jamii na  amezitaka taasisi zote za Umma kufanya manunuzi yote katika mfumo wa NeST.

Vile vile Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru ametembelea barabara na kuzindua mradi wa maji pamoja na kutembelea mradi wa Vijana Bodaboda ni Ajira Kashanda huku akipokea taarifa mbalimbali za utekelezaji wa ujumbe wa bio za Mwenge wa Uhuru 2024.

Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukabidhiwa  kukesha katika eneo la standi ya Kwenda na Kukabidhiwa  Mapema kesho Novemba 26, 2024 katika Shule ya Msingi Kyaka-Kyaka kwaajili ya kukimbizwa katika Wilaya ya Missenyi

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO LA UTOAJI WA VITAMINI A NA UPIMAJI WA HALI YA LISHE KWA WATOTO WA UMRI KUANZIA MIEZI 6 HADI 59 November 27, 2023
  • TANGAZO LA MABADILIKO YA BEI YA USHURU WA MKUNGU WA NDIZI December 31, 2023
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • MNASTAHILI PONGEZI KWA USIMAMIZI, UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 07, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA KYERWA

    April 29, 2025
  • TUNAPASWA KUULINDA MUUNGANO WETU-DC. MSOFE

    April 26, 2025
  • ‘TAULO HIZI ZITAWASAIDIA WATOTO KUSOMA KWA UHURU NA UTULIVU’

    March 07, 2025
  • Tazama vyote

Video

Kamati ya siasa ukaguzi wa Miradi Kyerwa
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved