• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

MKUU WA WILAYA KYERWA AHUTUBIA BARAZA LA MADIWANI

Imewekwa tarehe: August 3rd, 2023

MKUU wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe leo tar. 03 Agasti 2023 amehutubia baraza la Madiwani katika kikao cha robo ya nne ya baraza hilo kilichofanyika katika ukumbi wa Rweru Plaza Wilaya ya Kyerwa.

Akizungumza katika baraza hilo Mhe, Msofe amewapongeza Waheshimiwa Madiwani na Watumishi wa Halmashauri kwa kukusanya mapato na kuvuka lengo hadi kufikia asilimia 149 za makadirio ya mwaka wa fedha wa 2022/2023 na kuwataka kuongeza juhudi katika ukusanyaji na kuibua vyanzo vingine vya mapato katika Wilaya ya Kyerwa.

Vile vile amewataka Waheshimiwa Madiwani wasimamie mapato kwa uadilifu na kuwakumbusha wajibu wa kusimamia miradi inayotekelezwa katika maeneo yao kwa kuwa wao wanajukumu la kukagua na kusimamia miradi hiyo ili isihujumiwe.

Aidha amewataka waheshimiwa madiwani kuendelea kusisitiza suala la lishe katika kata zao ili kuondokana na utapiamlo unayoisumbua jamii ya Kyerwa. Huku akisisitiza  utunzaji wa mazingira katika jamii, hasa kuzuia uchomaji wa moto unaondelea kufanyika katika maeneo mbalimbali na kuvitaka vyombo vinavyohusika kuwachukulia hatua stahiki wale ambao wanafanya uharibifu huo.

Awali akitoa hotuba yake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa Mhe. Bahati Henerico amesema Wilaya ya Kyerwa iliidhinishiwa kutumia kiasi cha Sh 39,404,217,740.00 kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli mbalimbali za halmashauri zikiwemo kulipa mishahara, matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo ambacho kiasi hicho kimetumika kwa asilimia 100.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kyerwa Mhe. Innocent  Bilakwate amewapongeza; Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti  wa Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji na watumishi wa halmashauri, vyombo vya ulinzi na usalama na taasisi za serikali kwa kushirikana na Waheshimiwa Madiwani kwa kupambana na magendo ya kahawa iliyokuwa ikitoroshwa na kupelekwa nchi za nje na kupelekea  kukuza pato la wilaya ya Kyerwa na kuahidi kuendelea kushiriana nao.

Aidha wataalamu kutoka idara mbalimbali za Halmashauri, RUWASA na TARURA waliwasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi na shughuli zao kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ambazo zilipokelewa na baraza hilo la madiwani katika wilaya ya Kyerwa.

Matangazo

  • TAARIFA YA FEDHA YA MWAKA 2024/2025 August 02, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPATIWA MAFUNZO

    August 04, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAKIPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 31, 2025
  • NG’OMBE 93,984 KUPATIWA CHANJO KYERWA

    July 24, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI RUKURAIJO

    July 23, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved