• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

MICHE YA KAHAWA MILIONI 1.7 KUGAWIWA WILAYANI KYERWA

Imewekwa tarehe: October 2nd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe leo tarehe 2 Oktoba 2023 amezindua zoezi la ugawaji wa miche ya kahawa kwa wakulima katika Kijiji cha Karenge Kata Isingiro Wilaya ya Kyerwa.

Katika uzinduzi huo Mhe. Mkuu wa Wilaya amewataka wakulima kuwa wazalendo na kwenda kuipanda katika mashamba yao na kuwaonya wale ambao wanania ya kwenda kuuza miche hiyo kwa watu wengine au nje ya nchi.

“Serikali inagawa miche hii kwa wakulima lengo si kwenda kuuza, unapopewa miche hii naamini unaeneo la kwenda kupanda lakini kama haitoshi wapo watu ambao huchukua hatua ya kwenda kuuza miche hii, nitamke wazi kwamba atakapobainika mtu tusilaumiane. Kwa hilo serikali haina masihara.

Tunawapenda wananchi wetu, tunapenda mkuze vipato, mbadilishe maisha yawe mazuri na huduma inayotolewa hapa ni kwa Watanzania na si vinginevyo, kama unategemea kwenda kuuza acha kwa sababu tutafuatilia” ameeleza Mhe. Msofe.

Awali akitoa taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kyerwa iliyosomwa na Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Bw. Meshack Libent amesema Wilaya ya Kyerwa imeotesha Miche 1,766,500 ambayo inatarajiwa kugawiwa kwa wakulima wa Wilaya ya Kyerwa Mwaka huu.

Aidha amesema wakulima watakaopatiwa miche hiyo ni wale waliojiandikisha kwa viongozi wa Kata au AMCOS zao na Mkulima atatakiwa kwenda na fomu iliyosainiwa na viongozi hao ili aweze kupatiwa miche na zoezi hili litaendelea hadi tar. 16/10/2023.

Vile vile ameeleza kuwa Wilaya imekusanya tani 38,652 za kahawa mwaka 2022/2023 na bado makusanyo yanaendelea na imejiwekea mikakati ya kukusanya tani 45,000 ifikapo 2025 ikiwa ni pamoja na kuendelea kuzalisha miche bora ya Kahawa.

Pia Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Kyerwa Mhe. Bahati Heneriko ametoa wito kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika sekta ya viwanda ili kuongeza thamani ya zao hilo.  

Matangazo

  • TAARIFA YA FEDHA YA MWAKA 2024/2025 August 02, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPATIWA MAFUNZO

    August 04, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAKIPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 31, 2025
  • NG’OMBE 93,984 KUPATIWA CHANJO KYERWA

    July 24, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI RUKURAIJO

    July 23, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved