• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

MABIRA SEKONDARI YAPONGEZWA

Imewekwa tarehe: September 1st, 2023

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Mussa Gumbo leo 1 Septemba 2023 ameshiriki katika hafla ya kuwapongeza Walimu wa Shule ya Sekondari Mabira iliyoandaliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa kwa ajili ya kuwapongeza na kuwapa motisha walimu wa shule hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, Mhe. Gumbo amewapongeza walimu wa shule hiyo kwa kufaulisha wanafunzi wote na kuupongeza uongozi kwa kuwa na ushirikiano ambao umepelekea ufaulu huo na kushika nafasi ya tatu katika Mkoa wa Kagera kwa shule za serikali.

Aidha amewataka waalimu pamoja na wanafunzi kuendelea kujituma zaidi ili kuendelea kufanya vizuri huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Wanamabira na kumuagiza Mkurugenzi Mtendaji kuipa kipaumbele Shule ya Sekondari ya Mabira kwa kutenga fedha za mapato ya ndani na kutatua changamoto za shule hiyo ikwemo ya mabweni na uzio wa shule hiyo.

“Pamoja na shule kufanya vizuri walimu mnanafasi kubwa katika jamii kwa kuchunga maadili, kwani mnajua wanafunzi wanatoka kule majumbani na kuja shule, niwaombe muendelee kufuatilia mienendo na tabia za wanafunzi wetu,” Amewaasa Mhe. Gumbo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa Mhe. Bahati Henerico ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano na serikali na Wataalamu wa Halmashauri kwa kusimamia fedha za miradi ya maendeleo ili iweze kuwanufaisha wananchi wa Kyerwa.

Mhe. Bahati ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka miwili, Wilaya ya Kyerwa tayari imeanzisha shule kumi za kidato cha tano na sita na kuwataka walimu wa shule ya Sekondari Mabira kujitahidi kufanya kazi kwa bidii ili kuendelea kuwa mfano kwa shule zingine mpya za kidato cha tano na sita katika Wilaya ya Kyerwa.

Akitoa neno la utangulizi Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Mwl. Stephano Ndabazi amesema shule hiyo ambayo imetoa wahitimu wa kidato cha sita kwa mara ya kwanza ilifaulisha wanafunzi wote; kwa daraja la kwanza 42, daraja la pili 26 na daraja la tatu alikuwa mwanafunzi mmoja tu, na shule hiyo changa kushika nafasi ya  tatu katika mkoa wa kagera kwa shule za sekondari za serikali.

Katika hafla ya utoaji motisha kwa waalimu waliofaulisha  wanafunzi katika mtihani wa taifa, kidato cha sita Mei 2023,  katika Shule ya Sekondari Mabira Walimu wote walipewa zawadi, ikiwemo fedha tasmu Pamoja na vyeti ikiwa ni njia mojawapo ya kuwapa motisha wa kuendelea kujituma huku walimu waalikwa  wa shule nyingine za Sekondari za Wilaya ya Kyerwa wakitakiwa kuiga na kujifunza kwa kile walichokifanya walimu wa  Shule ya Sekondari Mabira.

Matangazo

  • TAARIFA YA FEDHA YA MWAKA 2024/2025 August 02, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPATIWA MAFUNZO

    August 04, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAKIPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 31, 2025
  • NG’OMBE 93,984 KUPATIWA CHANJO KYERWA

    July 24, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI RUKURAIJO

    July 23, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved