• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

KYERWA YAADHIMISHA SIKU YA FIMBO NYEUPE DUNIA KATIKA KATA YA RUKULAIJO

Imewekwa tarehe: November 29th, 2017

Maadhimisho ya siku ya fimbo nyeupe duniani kwa Wilaya ya kyerwa yamefanyika leo tarehe 28 Novemba,2017 katika kata ya Rukulajo.Siku hii ni maalumu ambayo huadhimishwa kote ulimwenguni kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa macho (hasa wale waliopoteza uoni, yaani wasioona).Fimbo nyeupe, ni fimbo maalumu inayotumika na mtu asiyeona, ilikumtambulisha kwa watumiaji wengine wa barabara , wakati wowote na hasa anapokuwa akitembea.Katika kuadhimisha siku hii mgeni rasmi mheshimiwa Kanali Mstaafu Shaban I.Lisu -Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa alisisitiza wasioona wasinyanyapaliwe katika nyanja zote na aliahidi kutoa fimbo nyeupe moja kwa wasioona.Aidha naye kaimu mkurugenzi wa Halmashauri Mhandisi Juma Magotto aliahidi kutoa jumla ya fimbo nyeupe tatu kwa walemavu wa macho walioshiriki maadhimisho hayo.

Katika sherehe hii,shughuli mbalimbali zilifanyika,ikiwa ni pamoja na kusoma risala ambayo ilisomwa na ndugu Verena Goldian ambaye ni mlemavu wa macho kutoka kata ya Isingiro ambaye alishukuru jinsi Serikali inavyowasaidia kupata fursa za elimu kupitia shule na vyuo maalum kwa watu wasioona kama shule ya sekondari Mabira,shule ya Msingi Kihanga zilizopo hapa Wilayani.Aidha vyuo vya ufundi stadi vya Korogwe na Sengerema vimekua na mchango mkubwa katika kuwanoa walemavu wasioona.Shughuli nyingine zilizofanyika katika kilele hicho ni maigizo ya changamoto na umuhimu wa fursa za kielimu yaliyoonyeshwa na wanafunzi wa shule ya Msingi Nyabikurungo,ushonaji wa nguo na vitambaa yaliyoonyeshwa na mshiriki asiyeona ndugu Verena Goldian.

Lengo la maadhimisho ya siku hii, ni kuihamasisha jamii na watumiaji wote wa barabara kama vile madereva, kuiheshimu fimbo nyeupe na kumsaidia asiyeona anapotembea na anapovuka barabara. Pia siku hii hutumika kutambulisha shughuli mbalimbali zinazofanywa na wasioona, malengo yao, mahitaji yao, uwezo wao katika suala zima la maendeleo, changamoto wanazokabiliana nazo, na mchango unaohitajika toka Serikalini na wadau wengine wa maendeleo.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Mkataba wa Marrakesh uondoe vikwazo vya kusoma kwa wasioona”. Marrakesh ni mji katika nchi ya Morocco ambapo Serikali ya Tanzania iliridhia mkataba wa Kimataifa ili kutatua changamoto zinazowakabili watu wasioona ili nao wawe chachu ya kasi ya maendeleo nchini.Mkataba huu unataka kuchapwa kwa majarida ya nuktanundu au kuwekwa kwa sauti ili kuwasaidia watu wasioona kusoma na kupata taarifa mbalimbali.

Jumla ya washiriki takribani 250 walishiriki katika kilele cha maadhimisho ya siku hii.

Matangazo

  • TAARIFA YA FEDHA YA MWAKA 2024/2025 August 02, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPATIWA MAFUNZO

    August 04, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAKIPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 31, 2025
  • NG’OMBE 93,984 KUPATIWA CHANJO KYERWA

    July 24, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI RUKURAIJO

    July 23, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved