• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

KYERWA: WANANCHI WANEEMEKA, KUGAWIWA MICHE YA KAHAWA ZAIDI YA MILIONI 5 BURE

Imewekwa tarehe: October 17th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa,  imezindua  zoezi la ugawaji wa miche  ya Kahawa 5,161,666 kwa wakulima katika msimu wa mwaka 2025/2026 leo tarehe 17 Oktoba 2025 katika kitongoji cha Karenge Kijiji cha Karukwanzi Kata ya Isingiro.

Akizindua zoezi hilo Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, Mhe. Zaituni Msofe ameipongeza Halmashauri ,Bodi ya Kahawa  pamoja na sekta binafsi kwa kuendelea  kushirikiana katika kuhakikisha wanazalisha miche bora ya kahawa itakayo wanufaisha wakulima wa Wilaya ya Kyerwa.

Akizungumza na wakulima waliojitokeza katika zoezi hilo Mhe.Msofe amewataka Maafisa Kilimo kuweka utaratibu wa  ufuatiliaji wa wakulima baada ya zoezi la ugawaji wa miche ili kuhakikisha miche hiyo inaleta manufaa kwa wakulima.

“Tuwafikie wakulima tuwashauri vizuri ili sasa miche hii tunayoigawa iende ikatunzwe na iweze kukua hatimaye tupate faida na lengo tulilolikusudia tuweze kulipata” ameeleza Mh. Msofe.

Naye Bw. Meshack Libent, Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi  amesema kuwa mwaka huu miche imeongezeka ukilinganisha na miaka ya nyuma hivyo kutakuwa na ongezeko la ugawaji wa miche na kutoa rai kwa wakulima kutumia mvua za vuli na kuhakikisha wanapanda miche yao, kwa kuwashirikisha maafisa ugani.

Dr. Albert Katagira, Mkurugenzi wa  JJAD, kampuni inayojishughulisha na kilimo cha kahawa  amesema miche hiyo ni bora na inachukua muda mfupi kwa kuanza kutoa mazao kwa mwaka mmoja "Miche hii ni bora na ya  kisasa, wananchi ni mashahidi, kwa waliochukua mwaka juzi na mwaka jana, wamenufaika.”

Kwa upande wake Bi. Mary Clemence mkulima wa kahawa katika Kata ya Isingiro ameishukuru Serikali pamoja na Halmashauri kwa kuzindua  zoezi hilo la ugawaji wa miche bora ya kahawa, kwani kupitia kilimo cha kahawa kimewasaidia wanawake wengi katika kutengeneza Uchumi wao binafsi.

Pia Bw. Tumaini clavery, ameishukru na kuipongeza Serikali kwani kupitia zao la kahawa vijana wengi wameweza kujikwamua kiuchumi.








Matangazo

  • TANGAZO LA KUKODISHA GARI August 27, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • WAZEE NI TUNU YA TAIFA TUWALINDE-MHE. MSOFE

    October 18, 2025
  • KYERWA: WANANCHI WANEEMEKA, KUGAWIWA MICHE YA KAHAWA ZAIDI YA MILIONI 5 BURE

    October 17, 2025
  • MAFUNZO YA VITENDO KWA WATAALAM WA WAFYA YA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO

    October 16, 2025
  • WATAALAM WA AFYA WANOLEWA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO

    October 13, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved