• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

KAMATI YA CCM YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI WILAYANI KYERWA

Imewekwa tarehe: July 14th, 2023

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kyerwa imetembelea na kukagua miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Bilioni tano inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi. 

Akiongoza ziara hiyo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Ndg. Daniel Damiani amesema ameridhishwa na usimamizi wa miradi ambayo inatekelezwa katika Wilaya ya Kyerwa na kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji na Wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa juu ya kumalizia miradi hiyo.

“Miradi yote tuliyoitembelea imesimamiwa kwa ubora, imesimamiwa vizuri na imejengwa kwa viwango na tunaagiza shule za sekondari mbili kufikia mwaka kesho ziwe zimesajiliwa na zianze kupokea wanafunzi na wananchi wajue faida ya kuendelea kuchangia zile sekondari kwa vile zitaondoa msongamano katika shule mama za wilaya yetu.” Alisema Damiani. 

 Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Kyerwa Mhe. Innocent Bilakwate amempongeza Mkurugenzi Mtendaji pamoja na timu nzima ya halmashauri kwa kudhibiti utoroshaji wa kahawa na kuongeza ukusanyaji wa mapato amabayo yanasaidia kukamilisha miradi kwani kipindi cha nyuma kulikuwa na maboma yaliyotelekezwa na wasimamizi jambo ambalo lilikuwa linarudisha nyuma maendeleo ya wilaya.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Bahati Henerico amesema halmashauri wamejipanga katika kukusanya na kusimamia mapato na fedha inayopatikana itapelekwa katika miradi ya maendeleo na kuwataka wananchi waendelee kushiriki katika maendeleo ya wilaya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa SACF. James John amesema kwa mwaka  wa fedha uliopita serikali ilitoa zaidi ya Bilioni 38 kwa matumizi ya kawaida ya miradi ya maendeleo katika wilaya ya Kyerwa, na amepokea maelekezo yote ya chama na yatafanyiwa kazi.

Katika ziara hiyo kamati ya CCM Wilaya ya Kyerwa imetembelea miradi mitano  ambayo ni mradi wa hospitali ya wilaya ambao umegharimu kiasi cha shilingi 2,100,000,000/= na ulianza kutoa huduma mwaka 2020, mradi wa ujenzi wa  chuo cha VETA ambao umeanza kutekelezwa Juni 2023 wenye thamani ya Bilioni tatu.

Pia ujenzi wa shule ya msingi mpya ya mwangaza iliyopo kata ya Kikukuru, kijiji cha Mukunyu wenye thamani ya kiasi cha shilingi 540,300,000/=.  Mradi wa shule ya sekondari Makazi uliopo kata ya Mabira ambao vyumba vitatu vya madarasa na ofisi moja vimekamilika na vimegharimu shilingi 80,973,881/=

Pamoja na mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Umoja iliyopo kata ya Rwabwere kijiji cha Umoja  wenye thamani ya shilingi 44,939,600/= ambao ujenzi wa vyumba vitatu  vya madarasa viko katika hatua ya umaliziaji.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI MBALIMBALI June 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • KYERWA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • NI SWALA LA KUAMUA TU, SISI WANAKYERWA HATUTAKI UCHAFU

    May 31, 2025
  • DC AFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

    May 29, 2025
  • TUSHIRIKIANE KUPAMBANA NA MAGENDO YA KAHAWA-DAS KYERWA

    May 14, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved