• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

HALMASHAURI KUU YA CCM KYERWA YAPOKEA TAARIFA YA ILANI YA UCHAGUZI

Imewekwa tarehe: February 19th, 2024

Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kyerwa leo Tar. 19 Februari 2024 imepokea taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2020/2025 kwa kipindi cha Julai hadi Disemba 2023 katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Kyerwa.

Taarifa hiyo imewasilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe katika kikao hicho ambayo imeeleza juu ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo zinazofanywa na serikali katika Wilaya ya Kyerwa.

Mkuu wa Wilaya ameeleza shughuli za Idara na Vitengo pamoja na taasisi za Serikali katika utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Sekta ya Elimu, Afya, Kilimo na Umwagiliaji, Mifugo na Uvuvi, utawala na utumishi, TEHAMA, ardhi, uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, Wakala wa Maji, Umeme pamoja na barabara.

Aidha amekishukuru Chama cha Mapinduzi kwa ushirikiano kinachotoa kwa Serikali katika Wilaya ya Kyerwa “Niwashukuru viongozi wangu wa Chama kwa maana ya kwamba tumekuwa tukishirikiana bega kwa bega, pale ambapo kuna changamoto tunaitana tunaelekezana tunasonga mbele. Ushirikiano wa Chama na Serikali ndio yametufikisha hapa tulipo. Niwaombe tuendelee kushirikiana na tuendelee kuchapa kazi” amesema Mhe. Msofe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya Kyerwa Ndg. Daniel Damiani amesema wameridhishwa na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kumpongeza Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji, Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa na Taasisi nyingine za Serikali na kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika kuendelea kuijenga Wilaya ya Kyerwa.

Aidha Mwenyekiti huyo amewatunuku vyeti vya utendaji kazi mzuri na kutoa huduma kwa wananchi wa Wilaya ya Kyerwa kwa Mhe. Zaituni Msofe-Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, Mhe. Bahati Henerico-Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa na SACF. James John-Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa.

Kwa Upande wake Mbunge wa Jimbo la Kyerwa Mhe. Innocent Bilakwate amesema ataendelea kuisemea Wilaya ya Kyerwa katika ngazi ya juu ili iweze kusonga mbele huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ya Wilaya ya Kyerwa katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Matangazo

  • TAARIFA YA FEDHA YA MWAKA 2024/2025 August 02, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPATIWA MAFUNZO

    August 04, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAKIPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 31, 2025
  • NG’OMBE 93,984 KUPATIWA CHANJO KYERWA

    July 24, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI RUKURAIJO

    July 23, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved