• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

HAFLA YA UTOAJI TUZO KWA UFAULU BORA KIDATO CHA SITA 2024

Imewekwa tarehe: August 3rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe ametoa tuzo za ufaulu bora wa kidato cha sita mwaka 2024 kwa walimu kwa kuzingatia hali ya ufaulu katika masomo wanayoyafundisha.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya amewapongeza Walimu na watahiniwa wote waliofanya vizuri katika mtihani wao wa kidato cha sita kwa kupata daraja la kwanza.

Aidha amempongeza Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa SACF. James John kwa kuwa na utaratibu wa kuandaa hafla ya utoaji tuzo za ufaulu bora kwa walimu na wanafunzi kwani huongeza morali kwa walimu na wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao.

Hafla hiyo imefanyika katika Shule ya Sekondari Mukire, ambayo imeshika nafasi ya kwanza kiwilaya na kimkoa na nafasi ya 35 kitaifa, baada ya watahiniwa wote 45 kupata ufaulu wa daraja la kwanza (division one).

Shule hiyo imetunukiwa zawadi ya ngao ya ufaulu bora huku Mkuu wa Shule na walimu waliofaulisha katika masomo yao kwa wanafunzi kupata gredi A hadi C kutoka katika shule zingine nne za Serikali, walipokea tuzo za vyeti na fedha taslim. Aidha kwa kuzingatia pia ufaulu wa GPA kwa kila somo, walimu wanne wenye ufaulu wa juu, kupita wenzao, walipokea fedha taslim hadi shilingi laki saba kila mmoja.

Vile vile walimu wenye ufaulu bora kutoka shule zingine tano za Serikali zilizopo katika Wilaya ya Kyerwa ambazo ni; Isingiro, Nyabishenge, Kimuli na Mabira pamoja na shule mbili za binafsi za Kaisho na Kyerwa Bright Star walipokea tuzo za vyeti na fedha taslimu.

Awali akitoa taarifa ya ufaulu kwa ujumla, Afisa Elimu wa Wilaya Kyerwa Mwl. Ndabazi Stephano amesema, jumla ya shule saba zilifanya Mtihani wa Kidato cha Sita mwezi mei 2024 katika wilaya ya Kyerwa na matokeo ya watahiniwa wote wakipata Daraja la Kwanza na la Pili isipokuwa Mwanafunzi mmoja tu ndiye kapata Daraja la tatu.

“Kama Msimamizi wa idara, nawapongeza walimu na wanafunzi wote, kwa ufaulu mzuri, pia naipongeza OR Tamisemi kwa kubuni mkakati wa kusimamia shule kwa malengo mahsusi, yaani Key Performance Indicators (KPIs), Mkakati uliozaa matunda nchi nzima.

Kwa dhati, naishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za ujenzi wa miundombinu iliyopelekea Wilaya ya Kyerwa kusajili shule 10 za Kidato cha Tano na Sita ndani ya miaka miwili tuu, yaani mwaka 2021/22 na 2022/23.” Ameeleza Mwl. Ndabazi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa SACF. James John amewapongeza walimu na wanafunzi kwa ufaulu mzuri na ameahidi kuendelea kushirikiana na walimu, wazazi na wadau wa elimu ili kuongeza chachu ya ufaulu na hivyo kufikia matakwa ya mahiri zilizokusudiwa katika mitaala ya elimu.

Vile vile ameipongeza Bodi ya Shule na Jukwaa la Wazazi wa shule hiyo kwa kuendelea kujitolea na kuunga mkono juhudi za Serikali kwa Kuajiri walimu wa muda 20 na kujenga nyumba ya walimu ya two in one yenye thamani ya milioni 75.

Protenes Alexander, muhitimu wa Kidato cha sita 2024 ambaye amepata Division one ya point 6 amewashukuru walimu kwa ufundishaji na kazi kubwa waliofanya kuwafundisha na kuwaomba kuendelea na moyo huo huo huku akiwasihi wanafunzi wanaoendelea na masomo kuongeze bidi katika masomo yao.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kyerwa ambaye alitoa zawadi ya shilingi Milioni moja, Diwani wa Kata ya Kikukuru, Wenyeviti wa Bodi ya Shule, wazazi, Maafisa Elimu Kata wa Kata zote, wakuu wa shule za sekondari, na viongozi wa Chama cha Walimu Wakuu wa Wilaya ya Kyerwa na Mkoa wa Kagera pamoja na wageni mbalimbali.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI MBALIMBALI June 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • KYERWA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • NI SWALA LA KUAMUA TU, SISI WANAKYERWA HATUTAKI UCHAFU

    May 31, 2025
  • DC AFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

    May 29, 2025
  • TUSHIRIKIANE KUPAMBANA NA MAGENDO YA KAHAWA-DAS KYERWA

    May 14, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved