• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

DC APOKEA MPANGO WA CSR WA KIKAGATI

Imewekwa tarehe: April 16th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe amepokea mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (Cooperate Social Responsibility- CSR) wa Mradi wa Kufua Umeme wa Kikagati katika Kikao kilichofanyika leo Aprili 16, 2024 katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa.

Akiwasilisha taarifa hiyo, Afisa Kiungo Jamii wa Mradi huo Bi. Jacqueline Stewart amesema, kwa mwaka huu wamepanga kutekeleza shughuli mbalimbali za Uwajibikaji kwa Jamii ili kuendelea kusaidia jamii inayozunguka mradi huo na kutengeneza mahusiano mazuri na jamii hiyo.  

Bi Jacqueline amesema wamepanga kutoa huduma za elimu kwa jamii katika suala la usalama barabarani pamoja na usalama wa raia dhidi ya ukatili kwa kushirikiana na jeshi la polisi ili kupunguza ajali na vifo vinavyosababishwa na vyombo vya moto pamoja na ukatili wa raia unaotokea mara kwa mara katika jamii inayozunguka mradi huo.

Vile vile amesema watakuwa na programa ya afya kwa kutoa elimu juu ya kupima Maambuzi ya Virusi vya UKIMWI, ikiwa ni pamoja na kupima magonjwa ya kansa, TB na shinikizo la damu kwa lengo la kuimarisha afya za wananchi wa eneo hilo.

Pamoja na mambo mengine pia amesema wanaendelea na zoezi la uchakataji wa hati miliki za ardhi kwa wananchi nane wa upande wa Tanzania waliohamishwa katika maeneo yao na kupata sehemu nyingine ili waweze kuyamiliki kihalali ikiwa ni pamoja na  Kuongeza huduma za maji kwa kushirikiana na RUWASA, pamoja na utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti katika maeneo hayo.

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe amewashukuru kwa mipango mizuri na ambayo itawasaidia wanakyerwa kwa kuwa salama hasa katika elimu ya usalama barabarani na elimu ya usalama wa raia ambayo itatolewa kwa jamii ya wanakyerwa wanaozunguka maeneo ya Mradi.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Katibu Tawala, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa pamoja na Wataalam mbalimbali kutoka ofisi za umma katika Wilaya ya Kyerwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI MBALIMBALI June 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • KYERWA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • NI SWALA LA KUAMUA TU, SISI WANAKYERWA HATUTAKI UCHAFU

    May 31, 2025
  • DC AFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

    May 29, 2025
  • TUSHIRIKIANE KUPAMBANA NA MAGENDO YA KAHAWA-DAS KYERWA

    May 14, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved