• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

BASHUNGWA AMKABIDHI MKANDARASI UJENZI WA BARABARA KYERWA - OMURUSHAKA

Imewekwa tarehe: October 18th, 2024

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemtambulisha kwa Wananchi na kumkabidhi eneo la mradi Mkandarasi Kampuni ya  Shandong Luqiao Group atakayeanza ujenzi wa barabara ya Kyerwa - Omurushaka (km 50) kwa kiwango cha lami na kumuagiza  Wakala ya Barabara (TANROADS) kumsimamia Mkandarasi huyo ili barabara hiyo ikamilike kwa wakati bila ya kusuasua.

Hafla ya kumkabidhi Mkandarasi imefanyika leo 18 Oktoba 2024 katika eneo la Rwenkorongo Wilaya ya Kyerwa ambapo Bashungwa ameeleza ujenzi wa barabara utaziunganisha Wilaya za Karagwe na Kyerwa kwa kugharamiwa na Serikali kwa Shilingi Bilioni 94.34.

“Mheshimiwa Rais anatambua wanaKyerwa walikuwa  na kiu kubwa na barabara hii ndio maana ametoa kibali ili niweze kufika hapa na kumkabidhi Mkandarasi huyu kwenu ili aweze kuaza ujenzi na kuwaondolea wananchi kero ya usafiri mliyokuwa mnaipata”, amesisitiza Bashungwa.

Bashungwa ameeleza kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia Mkandarasi kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo iliyokuwa inaishia Kata Chonyonyo na kuunganisha kipande cha kilometa 11 hadi kufika Omurushaka ambapo TANROADS wanaendelea na taratibu za kimkataba.

Amesisitiza kuwa ujenzi wa barabara ya Kyerwa - Omurushaka utafungua fursa mpya za Kibiashara, Uchumi na Uwekezaji pamoja na kuchochea shughuli za utalii katika Mbuga za Taifa za Ibanda, Burigi Chato, Rubondo na Rumanyika zilizopo katika Mkoa wa Kagera na Geita.

Aidha, Bashungwa amebainisha mikakati ya Serikali ya kuendelea kuifungua Wilaya ya Kyerwa kwa barabara za lami ambapo ameeleza barabara Omurushaka - Kyerwa itakuwa na mwendeleo hadi Murongo (Km 112.11) na kuunganisha Mji wa Nkwenda na Nyakaiga pamoja na kupendezesha mji wa Isingiro na Nkwenda kwa barabara za lami.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Fatma Mwassa, amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa huo ikiwemo Sekta ya Afya, Elimu, Kilimo na Miundombinu ya barabara.






Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI MBALIMBALI June 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • KYERWA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • NI SWALA LA KUAMUA TU, SISI WANAKYERWA HATUTAKI UCHAFU

    May 31, 2025
  • DC AFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

    May 29, 2025
  • TUSHIRIKIANE KUPAMBANA NA MAGENDO YA KAHAWA-DAS KYERWA

    May 14, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved