• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 50.3

Imewekwa tarehe: February 4th, 2025

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa limeridhia kupitisha rasimu ya bajeti ya Shilingi 50,329,376,863.00 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 ambayo sawa na ongezeko la 14.9% ya bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo Halmashauri ilipitisha kiasi cha shilingi Bilioni 42.8 ambayo inaendelea kutekelezwa.

Akizungumza katika Mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe ameipongeza Halmashauri kwa kuandaa bajeti ambayo imegusa Nyanja zote za maendeleo na kutoa wito kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kasi ili kutoa huduma kwa wananchi huku akiitaka Halmashauri kuendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato.

“Tuna kila sababu ya kuendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato katika vyanzo tulivyo navyo, lakini pia tuna kila sababu ya kuendelea kubuni vyanzo vingine vipya vya kuendelea kuongeza mapato.” Amesema Mhe. Msofe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa Mhe. Bahati Henerico amesema bajeti hiyo itaenda kutekelezwa kama ilivyopangwa kwani atahakikisha anasimamia utekelezaji wa bajeti hiyo kama alivyosimamia bajeti zingine zilizopita ili kuendelea kuijenga Kyerwa.

Awali akiwasilisha rasimu ya bajeti hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, Mkuu wa Divisheni ya Mipango na Uratibu Ndg. John Msafiri, amesema Halmashauri inakadiria kupokea na kutumia jumla ya shilingi 50,329,376,863.00 kutoka katika vyanzo vya; mapato ya ndani shilingi 6,060,197,120,00 Ruzuku ya Serikali shilingi 37,450,477,743.00 na fedha za nje (Wahisani) 6,818,702,000.00 ambazo zitatumika katika kutekeleza shughuli za Halmashauri.

Aidha, Ndg. Msafiri amesema vipaumbele vya bajeti hiyo ni kujengea uwezo watumishi, Kuboresha shughuli za kilimo, Kusimamia mazingira na mabadiliko ya Tabia ya nchi, Kuwezesha ukusanyaji wa mapato na Kuboresha ustawi wa wananchi.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kyerwa Mhe. Innocent Bilakwate ameipongeza Halmashauri kwa kuandaa mpango mzuri wa Bajeti na kusema atasimamia na kuhakikisha bajeti hiyo inapitishwa katika ngazi zote zinazofuatia za Mkoa na Bunge.

Nao Waheshimiwa Madiwani wameonesha kuwa na imani na kuunga mkono mipango na bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 ikiwemo Baraza la wafanyakazi, kamati ya ukimwi, kamati ya elimu, kamati ya uchumi, ujenzi na mazingira, kamati ya fedha, Utawala na mipango.

Matangazo

  • TAARIFA YA FEDHA YA MWAKA 2024/2025 August 02, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPATIWA MAFUNZO

    August 04, 2025
  • MAAFISA MIFUGO WAKIPATIWA MAFUNZO YA MFUMO WA UFUATILIAJI NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 31, 2025
  • NG’OMBE 93,984 KUPATIWA CHANJO KYERWA

    July 24, 2025
  • MKUU WA WILAYA AFANYA ZIARA YA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI RUKURAIJO

    July 23, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved