Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya ya Kyerwa.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Bahati Henerico akiongoza ziara hiyo amesema wamejionea miradi inayotekelezwa kwa ufanisi, kasi na inaonekana italeta tija kwa Wanakyerwa pindi ikikamilika, kwani huduma zitasogezwa karibu na kuinua uchumi na maendeleo ya Wilaya ya Kyerwa.
Ujenzi wa Soko la kimataifa la Ndizi-Nkwenda wenye thamani ya bilioni 1.6 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2025, Ujenzi wa vyumba 15 vya Maduka Stendi ya Nkwenda vyenye thamani ya Milioni 97.5 na Ujenzi Jengo la Wodi ya Wazazi katika Zahanati ya Rukuraijo wenye thamani ya Millioni 280.
Miradi hiyo iko katika hatua mbalimbali ambayo imefanya Kamati kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa SACF. James John na Wataalam wake kwa usimamizi mzuri wa miradi hiyo inayotekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu na Mapato ya ndani ya Halmashauri.
Vile vile Kamati imetembelea eneo la uwekezaji la Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa lenye ukubwa wa Ekari 15 lililopo katika Kijiji cha Kyerwa na kupongeza mpango huo wa Halmashauri wa kuwa na eneo hilo na kutaka taratibu za utekelezaji wa mradi huo ziendelee.
Aidha Mhe. Bahati amesisitiza umuhimu wa uwazi, ushirikishwaji wa jamii na viongozi wa Vijiji ama maeneo husika, pamoja na matumizi bora ya rasilimali za umma kwa maendeleo katika utekelezaji wa miradi hiyo kwani inawahusu wao na wanahaki ya kujua kinachoendelea katika maeneo yao.
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved