• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

DC ASHIRIKI MDAHALO WA MIAKA 60 YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Imewekwa tarehe: April 25th, 2024

Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tar. 25 Aprili 2024 katika Wilaya ya Kyerwa umefanyika mdahalo maalum wenye mada mbalimbali zinazohusiana na muungano.

Wataalam kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, TARURA, RUWASA, TANESCO, TAKUKURU, TFS na Jeshi la Polisi waliwasilisha mada mbalimbali ambazo zilichangiwa na washiriki wa mdahao huo huku wanafunzi wakitoa burudani mbalimbali.  

Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mhe. Zaituni Msofe amewashukuru watumishi na wananchi kwa kushiriki kikamilifu maaadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia kwenye usafi wa mazingira na kupanda miti katika Shule ya Sekondari ya Kyerwa Modern, Kushiriki Dua na sala maalum, Michezo mbalimbali na uzinduzi wa chanjo katika Kata ya Isingiro, kushiriki usafi, kupanda miti na kutembelea wagonjwa katika Kituo cha Afya Nkwenda na kumalizia na mdahalo wa leo.

Aidha amesema kuna changamoto nyingi zimeshughulikiwa na zipo zinazoendelea kushughulikiwa ikiwemo barabara ya lami ya Omurushaka-Rwenkorongo ambayo tayari imesainiwa na muda wowote mkandarasi ataanza kazi ya kuitengeneza.

Vilevile amewataka Wanakyerwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya Sita kwa kuendelea kutunza miundombinu ya miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa ili iwezee kuinufaisha jamii ya sasa na vizazi vijavyo.

Pia amewataka Wanakyerwa kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa, kutunza mazingira kwa kupanda miti pamoja na kulinda Amani na usalama wa nchi.

Baada ya mdahalo huo, Mkuu wa Wilaya alijumuika na wananchi katika kufuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mubshara katika viwanja Rwenkorongo Kata ya Kyerwa.  

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru inasema, “miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tumeshikamana na Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa Letu.” 

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI MBALIMBALI June 30, 2025
  • TANGAZO LA KAZI KADA YA AFYA July 09, 2024
  • TANGAZO LA KAZI July 17, 2024
  • TANGAZO UPANGISHAJI WA FREMU ZA MADUKA KATIKA STENDI YA MABASI MAZIWA NKWENDA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 June 12, 2025
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • KYERWA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • NI SWALA LA KUAMUA TU, SISI WANAKYERWA HATUTAKI UCHAFU

    May 31, 2025
  • DC AFUNGUA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA

    May 29, 2025
  • TUSHIRIKIANE KUPAMBANA NA MAGENDO YA KAHAWA-DAS KYERWA

    May 14, 2025
  • Tazama vyote

Video

KUFUNGA MAFUNZO YA MGAMBO WILAYANI KYERWA
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved