Wednesday 13th, August 2025
@KATA YA RUKURAIJO
Siku ya fimbo nyeupe ni nini?
Ni siku maalumu ambayo huadhimishwa kote ulimwenguni kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa macho (hasa wale waliopoteza uoni, yaani wasioona).Fimbo nyeupe, ni fimbo maalumu inayotumika na mtu asiyeona, ilikumtambulisha kwa watumiaji wengine wa barabara , wakati wowote na hasa anapokuwa akitembea.
Lengo la maadhimisho ya siku hii, ni kuihamasisha jamii na watumiaji wote wa barabara kama vile madereva, kuiheshimu fimbo nyeupe na kumsaidia asiyeona anapotembea na anapovuka barabara. Pia siku hii hutumika kutambulisha shughuli mbalimbali zinazofanywa na wasioona, malengo yao, mahitaji yao, uwezo wao katika suala zima la maendeleo, changamoto wanazokabiliana nazo, na mchango unaohitajika toka Serikalini na wadau wengine wa maendeleo.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Mkataba wa Marrakesh uondoe vikwazo vya kusoma kwa wasioona”. Marrakesh ni mji katika nchi ya Morocco ambapo Serikali ya Tanzania iliridhia mkataba wa Kimataifa ili kutatua changamoto zinazowakabili watu wasioona ili nao wawe chachu ya kasi ya maendeleo nchini.Mkataba huu unataka kuchapwa kwa majarida ya nuktanundu au kuwekwa kwa sauti ili kuwasaidia watu wasioona kusoma na kupata taarifa mbalimbali.
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved