Wilaya ya Kyerwa, leo tarehe 26 Aprili, 2022 imeadhimisha sherehe za Muungano kwa kufanya usafi maeneo kadhaa ndani ya Wilaya. Zoezi la maadhimisho haya lilianzia eneo la ofisi za Halmashauri ambapo watumishi na wananchi walikusanyika mnamo saa 12 asubuhi kwa kufyeka nyasi na uokotaji wa takataka zilizokuwa mahali pasipostahili.
Aidha, baadae ya kufanya usafi kwenye ofisi za Halmashauri, watumishi na wananchi kwa umoja wao walielekea eneo la Rwenkorongo kujumuika na viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na wanachi wa Rwenkorongo kwa kufanya usafi maeneo ya pembezoni mwa barabara, eneo la Gulio/soko pamoja na mitaa ya viunga vya Rwenkorongo.
Aidha, katika kuhitimisha zoezi la usafi ambalo lilikamilika mida ya saa 4 asubuhi, Katibu Tawala wa Wilaya Mheshimiwa SI.Benjamin R Mwikasege aliwashukuru wananchi wote waliojitokeza kushiriki katika maadhimisho haya, na kuwasisitiza wajitokeze kwa wingi katika kushiriki zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linalotarajia kufanyika tarehe 23 Augosti, 2022. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa Ndugu SACF. James John alisema" Eneo la Rwenkorongo ni makao makuu ya Wilaya, hivyo wananchi wa eneo hili tujenge utamaduni wa kufanya usafi maeneo yetu kila siku, hii itasadia kuondokana na adui maradhi kutokana na uchafu".
Muungano wa Taganyika na Zanzibari uliasisiwa tarehe 26 Aprili, 1964 takribani miaka 58 iliyopita, na Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, na Hayati Abeid Aman Karume.
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved