Chama cha Skauti Wilaya ya Kyerwa,kimesajili jumla ya wanachama wapya 226 katika mahafali yaliyofanyika hivi karibuni, katika viwanja vya mpira wa miguu Isingiro.Katika mahafali hayo, yaliyohudhuriwa na Katibu Tawala Mkoa wa Kagera, Mheshimiwa Profesa Faustine Kamuzora , ambaye alikuwa mgeni rasmi,shughuli mbalimbali zilifanyika ikiwapo tukio la upandaji wa miti katika shule ya sekondari Isingiro.Aidha uapisho wa wanachama wapya wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Rashid Mwaimu, jumla ya wanachama 226 kutoka makundi ya Walimu wa shule za Msingi na Sekondari, Watendaji wa Kata, Wakuu wa Idara na Vitengo, Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya,Viongozi wa Chama na wananchi kwaq ujumla waliapa kiapo cha utii kujiunga na skauti,
Akiapisha wanachama hao, Kamishna wa Skauti Mkoa wa Kagera, Padre Marcel Rutakyamirwa aliwaasa wanachama wapya kutii na kuishi misingi ya skauti ili kuwa mabalozi wazuri katika kulinda na kuimarisha uzalendo kwa vijana wadogo. Aidha, naye Ndugu Flavius M.Kabalila akisoma risala kwa Mgeni rasmi alisema kuwa toka mwaka 2015 chama cha skauti Wilaya kimefanikiwa kupata ushindi wa nasafi ya kwanza kitaifa mfululizo mara tatu,kuanzisha makundi ya skauti kwa shule zote za Msingi na Sekondari Wilayani, na kuandaa vikosi vya Maafa na Uokoaji ngazi ya Kata.
Chama cha Skauti Kyerwa, kilianzishwa mnamo mwaka 2015 kikiwa na jumla ya wanachama 42 pekee, hadi kufikia sasa chama kimefikisha jumla ya wanachama 4,548.Matarajio ya chama kwa siku za usoni ni pamoja na kuanzisha mafunzo ya uongozi (PTC) kwa walimu walezi wa Skauti, kuendeleza mashirikiano kati ya Chama cha Skauti na TAKUKURU (TAKUSKA), na kuendesha mafunzo kwenye shule kwa kushirikiana na jeshi la Zimamoto.
Kauli Mbiu "Skauti be prepared"
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved