Kwa kuzingatia Mwongozo wa bajeti wa mwaka 2020-2021 , ilani ya uchaguzi, malengo ya maendeleo endelevu(SDG),mpango wa maendeleo wa taifa wa miaka 5, na dira ya maendeleo 2025,baraza la madiwani Halmashauri ya Kyerwa kwa pamoja limepitisha jumla ya shilingi 28,107,595,004.34 kama makisio ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2020/2021 katika kikao kilichofanyika leo tarehe 17.02.2020.
Akiwasilisha vipaumbele vya bajeti hii kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Afisa Mipango ndugu John Msafiri alisema kuwa Halmashauri imepanga kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato,kuimarisha huduma za afya kwa kuwezesha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba,kuimarisha huduma za elimu kwa kuwezesha mazingira bora ya kujifunza na kufundishia,kuimarisha huduma za kilimo na mifugo,kuboresha kiwango cha maisha kwa kuwezesha makundi maalum ya wanawake, vijana na wenye ulemavu, na kuimarisha mifumo ya usimamizi ,ufuatiliaji,tathmini na utoaji wa taarifa ili kuwezesha upatikanaji wa takwimu za kuwezesha kufanya maamuzi.
Aidha, kulingana mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2020/2021,Halmashauri inatarajia kutumia jumla ya 28,107,595,004.34 /= ambapo 974,320,000.00/=ni ruzuku ya matumizi ya kawaida, 18,707,379,000.00/= ni mishahara,3,577,664,009.34/= ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo toka serikali kuu,1,981,699,360/= ni makusanyo ya ndani, 1,569,032,635.00/= ni michango toka kwa wadau wa maendeleo,605,000,000.00 /= ni michango ya jamii, na 692,500,000.00/= ni fedha kutokana na CHF(Bima ya afya ya jamii), NHF(Bima ya serikali) na michango ya papo kwa papo tka kwenye vituo vya kutolea huduma.
Kwa mujibu wa bajeti hiyo, Halmashauri inataraji kupokea kiasi cha 23,259,363,009.34/= toka serikali kuu, 1,569,032,635.00/= toka wadau wa maendeleo, na kiasi cha 2,674,199,360/= kutokana na makusanyo ya ndani na 605,000,000.00 /=kutokana na michango ya wananchi.
Katika mpango huu, Halmashauri inatarajia kutekeleza miradi ya ujenzi wa mnada wa kimkakati wa mifugo katika mpaka wa Murongo, ununuzi wa boti kwa ajili ya kudhibiti uvuvi haramu,ujenzi wa soko la kimkakati la mazao ya biashara katika mji wa Murongo, na kuwezesha ujenzi wa maegesho ya magari katika miji ya Nkwenda, na Murongo
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved