Katibu Tawala wa Wilaya ya Kyerwa Bw. Mussa Gumbo leo Aprili 20, 2024 ameongoza zoezi la kufanya usafi wa mazingira pamoja na kupanda miti katika Shule ya Sekondari ya Kyerwa Modern ikiwa ni maandalizi ya maadhimisho ya miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26 mwaka huu.
Katika zoezi hilo, miti 250 imepandwa katika eneo la Shule ya Sekondari Kyerwa Modern iliyopo Kata ya Kyerwa pamoja na Miti 350 imepandwa katika eneo la Shule ya Msingi Kaaro Kata ya Nkwenda na kufanya jumla ya Miti 600 kupandwa leo katika Wilaya ya Kyerwa.
Akizungumza baada ya zoezi hilo Katibu Tawala amesema kuelekea miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wilaya imezindua kwa zoezi la kufanya usafi na kupanda miti na uhifadhi wa mazingira na kuhimiza juu ya utunzaji wa mazingira kwa kuendelea kupanda miti katika maeneo mbalimbali.
Katika zoezi hilo Katibu Tawala Bw. Gumbo, ameambatana na Diwani wa Kata ya Kyerwa Mhe. Aloyce Mafundi, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa Mwl. Mayala Sengerema, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Watumishi kutoka Halmashauri, Wataalam mbalimbali kutoka ofisi za umma, wananchi pamoja na wanafunzi.
Kauli mbiu ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru inasema, “miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tumeshikamana na Tumeimarika kwa Maendeleo ya Taifa Letu”.
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved