Kampeni ya Kitaifa ya chanjo ya matone inafanyika nchi nzima. Lengo la kampeni hii ni kuhakikisha tunazuia uingizwaji wa ugonjwa wa Polio nchini, kutokana na mlipuko wa ugonjwa huu uliotokea nchi za jirani za Malawi na Msumbiji. Wilaya ya Kyerwa imefanya uzinduzi huu tarehe 01 Septemba, 2022 katika Kituo cha Afya Nkwenda na kuzinduliwa na mgeni rasmi Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, Rashid Mwaimu. Zoezi la utoaji wa chanjo litafanyika kwa muda wa siku nne kuanzia tarehe 01 mpaka tarehe 4 septemba, 2022.
Akisoma taarifa kwa Mgeni rasmi, mratibu wa chanjo Wilaya, ndugu Awadhi Rushengo alisema kuwa chanjo ya Polio ni muhimu kwa ajili ya kinga kwa watoto wote wenye umri chini ya miaka 5. Aidha. Aliongeza kwa kusisitiza kuwa chanjo yam atone ya Polio ni kwa watoto wote waliowahi kupata na wasiopata chango hii hapo awali.
Naye Mheshimiwa Rashid Mwaimu aliwasisista wananchi wote wenye watoto chini ya umri wa miaka 5 kujitokeza, ili watoto wao wapatiwe chango na kuweza kufikia lengo la uchanjaji wa watoto 87,780 ndani ya Wilaya.
“Sisi kama Serikali, tumeishafanya maandalizi yote kwa ajili ya kuwapatia chanjo watoto wetu,niwahimize wazazi na walezi pelekeni watoto wenu kupatiwa chanjo katika vituo vya tiba na maeneo mbalimbali ambayo wataalam wetu wa Afya watakuwepo katika kutoa chanjo hii” Alisisistiza Mheshimiwa Mwaimu.
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved