Mkuu wa Wilaya ya KyerwaMhe. Zaituni Msofe leo tar. 15 Novemba 2023 amepokea taarifa ya utekelezaji wamradi wa kufua umeme wa kituo cha Kikagati Murongo ulioko mpakani mwa Tanzania naUganda unaotumia maji ya Mto Kagera.
Mradi huo ambao unazalishamegawati 14, ambazo saba huhudimia upande wa Tanzania na zingine saba huhudumianchi jirani ya Uganda unaendelea na huduma ya kutoa nishati hiyo ya umemepamoja na huduma nyingine za kijamii.
Akiwasilisha taarifa hiyo AfisaKiungo Jamii wa Kituo hicho Bi. Jackline Stewart amesema, miongoni mwa hudumahizo ni kutunza na kupanda miti katika eneo linalozunguka mradi, kuhamasishajamii kupanda miti, kufanya tafiti mbalimbali, kuwafuatilia na kuwahudumiawanufaika wa mradi ambao walilipwa fidia wakati wa uanzishwaji wa mradi nakujua hali zao.
Vile vile kufadhili masomona kutoa vifaa kwa vijana wanaozunguka mradi, kutoa elimu ya udhibiti wa taka,kutoa elimu za kijamii ikiwemo ya VVU na UKIMWI, pamoja na kutoa mikopo yenyeriba nafuu kwa wanachi wanaozunguka mradi huo.
Aidha Mkuu wa Wilayaamewashukuru na kuwapongeza kwa kuwajuza Wanakyerwa kinachoendelea katika mradihuo ikiwa pamoja na kutoa huduma ya umeme katika nchi ya Tanzania hasa Wilayaya Kyerwa na kuendelea kusaidia jamii inayozunguka mradi huo.
Wajumbe wengine wa Kikaohicho walikuwa ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kyerwa, Mwenyekiti wa Halmashauri,Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Wataalamu waHalmashauri na Wataalamu kutoka Ofisi ya Tanesco Kyerwa.
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved