Mheshimiwa Brigedia Marco Gaguti ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera,leo tarehe 9 Novemba, 2020 amegawa miche bora 300,000 ya Kahawa kwa wakulima.Mheshimiwa Gaguti aliyekuwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, mheshimiwa Rashid M. Mwaimu aliwapongeza wakulima wa Wilaya ya Kyerwa kwa kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa kutoka tani 56,000 kwa msimu wa mwaka 2019/2020 mpaka tani 74,000 kwa msimu wa mwaka 2020/2021.
Akihutubia katika mkutano uliofanyika katika kitalu cha miche cha Nyabikurungo, kilichopo kata ya Rukulaijo Wilaya ya Kyerwa, Mheshimiwa Gaguti alisema “Nawapongeza Chama cha ushirika cha Karagwe na Kyerwa (KDCU) na taasisi ya utafiti wa Kilimo ya TAKRI, kwa hatua ya kuwezesha wakulima kupata miche hii kupitia vyama vya msingi vya ushirika.Ni imani yangu miche hii, itaongeza tija na thamani kwa uzalishaji wa zao la Kahawa”.
Aidha, Meneja wa KDCU ndugu Oscar Dominic alielezea kuwa lengo la ugawaji wa miche hiyo ni kuongeza ubora na uzalishaji wa zao la kahawa kwa wakulima.
Wilaya ya Kyerwa ina jumla ya vyama vya ushirika 74 ambapo vipo chini ya mwamvuli wa chama kikuu cha ushirika cha KDCU.
Kyerwa District Council
Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA
Simu ya mezani: +255 686 397 972
Simu ya Mkononi: +255 754 422 746
Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz
Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved